Project Hope     uct >>stonecroft >> mwanamitindo wa kiafrika
Mwanamitindo wa Kiafrika:

Women's Empowerment  Program
Sports Bible Club
Living Water Bible Club

Huu mfumo wa kiafrica wa ambao ni wa kugawanya na kuzidisha ni muhimu kuliko wa kuongeza!

1. Mfumo huu utaanzishwa kwanza Tanzania kupitia, "Africa Training Bible School" (ATBS) ambao lengo lao la kwanza ni kuwa funza wachungaji kutoka makanisa 280 ambao wamo katika mpango wa ATBS ili wajiunge na masomo ya kibiblia ya Stonecroft. Watafundishwa kwa kupitia video na ktabu cha kiafrica cha kufundishia, hawa wachungaji watakuwa viongozi wa kwanza wa Stonecroft Tanzania, na Bwana akipenda kila mmoja wao atapatiwa kitabu ca utatu 10 - Mungu yukoje? 10 - Yesu ni nai? na 10 - Je Roho mtakatifu yuko wapi? Na kitabu ambacho kimejumuisha vitabu vyo hivi vitatu.

2. Hawa wachungaji watachukua taarifa hii na kwenda nayo katika vijiji vyao ambao nao watachagua mwanamke mmoja, labda kiongozi wa kinamama, na baada ya hapo atamfundisha huyu mama,na mchungaji atabaki kuwa mwangalizi wakufuatilia kazi inaendaje tu.

3. Watapatiwa kitabu cha mwongozo cha Stonecroft na vitabu 10 vya Stonecroft ‘Mungu anaonekanaje?’ vyote hivi vimetafsiriwa katika lugha yake anayo ielewa,na atapewa vitabu vingine 10, naye atatafuta wenzake 5 katika kanisa ili waanze kujifunza.
Na hawa 5 nao walete mmoja kila mmoja wao, katika huduma ya Stonecroft, na wataanza kujifunza utatu, ‘Mungu anaonekanaje?’ baada ya hapo ataendelea na "Yesu ni nani?” Na atahitimisha na "Roho mtakatifu yuko wapi?" Na atatumia videa na kitabu kuwafundisha ili nao wakawafikie wengine.

4. Na akifikia hapo atakuwa kiongozi wa wenzake hao 5. Na atakacho kifanya ni kurudia masomo ya Stonecroft kwa wanawake watano wengine tena kanisani hawa watano wa sasa watatiwa moyo kuwaletwa watu wasio okoka kanisani, sasa ataanza kuwafikia wasio fikiwa.

5. Mchungaji kwa wakati huu atakuwa ni mtu wa kutoa ushauri na mwangalizi.

6. Hawa viongozi wapya 5 pamoja na mwana maombi wao,watamtafuta mtu mmoja kanisani au kijijini ambaye ana sifa za kuwa kiongozi, wamfundishe kwa ruhusa ya mchungaji wao.

7. Kwa pamoja hawa wakina mama 5 watawasihi wasio mwamini Mungu wajiunge na masomo ya Stone croft,ya utatu, kwa kawaida kila mmoja awe na wakina mama 2, kumbuka masomo haya yawe na wakina mama10 - 12 women.

8. Wakisha kujifunza masomo haya ya utatu basi huyu mwangalizi atawafundisha wakina mama 2, mmoja toka kanisani kwake na mwingine kanisa jingine ambao watakuwa viongozi wa Stonecraft wa kizazi cha nne. Wana maombi wake watabaki na darasa hili katika kulifundisha.

9. Mtindo huu utandelea katika kanisa ambalo limejifunza mkakati huu.

10. Iwapo kuna swali ambalo huyu kiongozi hawezi kulijibu basi amuhusishe mwangalizi wake.

11. Kwa kadri muda unavyo zidi kuendelea tutapata waangalizi wengi zaidi kwa kadri mtandao huu unavyozidi kutanuka na video nyingi sana zitatengenezwa.

12. Kumbuka - kugawa na kuzidisha !

13. Kuzidisha ni bora kuliko kuongeza!

‘Uwe macho, Simama imara katika imani, Uwe jasiri,uwe mwenye nguvu. Fanya kazi zote kwa upendo ’

1 Corinthians 16: 13 – 14

 
     
Copyright ©  2023 www.UnitedCaribbean.com. All rights reserved. Disclaimer Click to Contact us