Project Hope     uct >> stonecroft >>  masomo ya biblia ya stonecroft
MASOMO YA BIBLIA YA STONECROFT:

Women's Empowerment  Program
Sports Bible Club
Living Water Bible Club

Karibu katika masomo ya kibiblia ya Stonecroft, tunajitahidi kumpatia kila mmoja neno la Mungu haijalishi ana kiwango gani katika safari hii ya Kiroho.

Ni maombi yetu kuwa masomo haya yatatoa fursa kwako ili upate kuwezeshwa na neno la Mungu ili uweze kuifikia jamii yako na injili ya Yesu Kristo.

MTAZAMO:
Masomo ya biblia ya stonecroft yaliandaliwa kwa msingi wa kufuatilia mikutano ya kuwafikia wasio fikiwa, lakini kwa sasa masomo haya yamekuwa mpaka kuwafikiwa magerezani na makanisani, maofisini, na maeneo mengine.

SIFA MUHIMU:
Masomo ya biblia ya Stonecroft yameandaliwa ili kufanya uinjilisti na uanafunzi, na injili hii imejumuishwa maeneo yote ambayo Stonecroft inafanya kazi.

Kila somo limeandaliwa maalum kabisa ili wale ambao hawamjui Mungu nao wapate kushiriki, kwa bahati mbaya wanawake wa Africa sio wote walio na biblia na ndio maan kulasa za biblia zimetolewa na kuacha vipengele vya biblia tu ili kuwawezesha nao kushiriki vizuri, na hii imeandaliwa katika mpangilio maalum wa kimatukio.

Masomo ya biblia ya Stonecroft yanaendeshwa katika nyumba, maeneo ya kazi, makanisani, mashuleni, hata chini ya mti katika vivuri huku Africa.

Masomo haya yameandaliwa katika, kufundisha juu ya kichwa furani cha somo lakini hata hivyo masomo yanayo husu vitabu vya biblia yanapatikana katika hatua ya juu.

Masomo ya biblia ya Stonecroft ni rahisi kujisomea katika makundi madogo na hata makundi makubwa, na masomo haya yanaanzia (4-14 masomo). Na utatu masomo 6 kwa hiyo kitabu kimoja kna masomo 18.

Masomo mengi yanakuwa na kitabu cha mwongozo wa masomo, kitabu hiki hutumika pamoja na biblia na kila anae shiriki masomo haya.

Majadiliano ni njia mojawapo katika ukuaji wa kiroho.

USHAURI WA KUJISOMEA:

Katika maeneo mengi ya Stonecroft washiriki hutumia kitabu cha mwongozo na biblia ya Kiswahili, ambayo hupatikana madukani, lakini kama nilivyosema kitabu cha mkononi cha biblia kinapatikana kwa wale wasio na biblia.

Vikundi hivi vya kujisomea hukutana mara moja kwa wiki, kwa dakika 60-90. Kama dakika ni chache kundi wanaweza kuamua kugawa masomo haya nusu, kwa kugawana maswali na kusoma andiko.ili kutanua kazi ya uanafunzi tunashauri kuwa vikundi lazima vitafute njia za kuongeza washiliki ili ufanisi wake uonekane katika jamii.

MAELEZO YA MASOMO:

Kuna aina tatu za masomo ya biblia ya Stonecroft:

• Masomo ya Utangulizi wa utatu.

• Masomo ya wakristo wanao kuwa.

• Na masomo yahusuyo vichwa vya somo.

Stonecroft waanze na somo la Utangulizi, ambalo linasema “Yesu ni nani?”, 'Mungu yukoje?’ na 'Je Roho mtakatifu yuko wapi?' Haya ni masomo muhimu sana kwa wakristo wapya na hata wale wa zamani maana ni muhimu hata kwa wale wanao taka majibu ya maswali yao. Haya masomo yote yamekwisha tafsiliwa Kiswahili na kazi bado inaendela ya kutafsiri huko Congo na Malawi pia.

 
     
Copyright ©  2023 www.UnitedCaribbean.com. All rights reserved. Disclaimer Click to Contact us