Project Hope     uct >> stonecroft >>wakati wa masomo 
WAKATI WA MASOMO:

Women's Empowerment  Program
Sports Bible Club
Living Water Bible Club

Mara zote anza masomo haya kwa maombi, ikiwa kama kuna mtu ana hoja basi kundi liandike hiyo hoja yake na mtaiombea katikati mwa juma.

Ikiwa kama hitaji lake ni maombi ya dhalula basi yajumuishwe siku hiyo hiyo.

Kumbuka kila mara uanzapo somo la “Yesu ni nani” kila mshiriki ataandika jibu lake katika kijitabu cha kujisomea, na uwakumbushe kuwa ni vizuri wakawa wanajaza majibu kabla ya kuja darasani.

Soma na kuwapatia washiliki maelezo katika mtindo wa uwazi huku ukiwangalia usoni, Kiongozi huwa najifunza na kusoma na kundi lote la washiriki, hutakiwi kuwa umeisimea sana biblia.

KIONGOZI ANAHAKIKISHA NAFASI NA SAUTI HUTUMIKA VIZURI KATIKA KUJISOMEA:

• Kuanza na kumaliza kwa muda mzuri, kumbuka masomo haya ya biblia yatakuwa pamoja na shule ya kuwawezesha wanawake.ambao watahitajika kwenda kushona.

• Tumia kitabu cha kiongozi na biblia ya Kiswahili hakita hitajika ktabu cha ziada.

• Watie moyo kila mtu ili ashiliki katika kujadili, na hakikisha hakuna ambaye anaongea kuliko wenginehakikisha unawatia moyo unapowasihi wajadili.

• Mtazamo wako umuelekee Yesu, na usijadili misimamo ya mafundisho ya kikanisa,au misimamo ya kisiasa, maswali ya misimamo na mafundisho ya makanisa yashughurikiwe maeneo mengine.

Tafuta watu ambao watakuwa viongozi wa baadae wa kundi.
Kama kiongozi ni lazima uwe mifano wa kundi, hakikisha watu hawajadili mambo ambayo yanapaswa kuwa siri, kwa mfano mambo yale ya nyumbani.uombe pamoja nao na kuwasihi watafute mwongozo wa Mungu.

Baada ya masomo ya Stonecroft yakina mama kufikia tamati, kila mtu ambaye anaoneka kuwa ni kiongozi basi apitie mafunzo maalum ya uongozi, kwa kutumia video na kitabu maalum cha uongozi, ili waweze kupeleka stonecroft nyumbani kwao. Na katika makanisa yao.

Uwaulize washiriki wafikilie watu ambao wanaweza kuwaarika, uwahimize waanze kuwaarika watu katika masomo, na pia waanze kuwaombea kwa kuwataja majina yao.

Mambo muhimu ya kukumbuka.

• Iwapo huwezi kuongoza masomo haya ya biblia kwa sababu yeyote ile, basi kiongozi aliyethibitiswa aje na kuchukua nafasi hiyo.

• Hutakiwi kumpatia mwenzako kitabu cha mwongozo mtu yeyote Yule hata kama uko nae katika dara moja.

 
     
Copyright ©  2023 www.UnitedCaribbean.com. All rights reserved. Disclaimer Click to Contact us