Project Hope     uct >>stonecroft >>uongozi
UONGOZI WA STONECROFT:

Women's Empowerment  Program
Sports Bible Club
Living Water Bible Club

Viongozi wa Stonecroft wanafanya majukumu yao katika ofisi ya kitaifa na hata kazi ambazo ziko mbali na hapo.

Lorraine Potter Kalal: Raisi

Lorraine Potter Kalal Huduma yake iliyo jawa na mafanikio, Pamoja na upendo wake wa Stonecroft na maono na historia, Yeye kama raisi hujiona kuwa ndie Mtumwa mkubwa, Lorrain anahitaji kuona kuwa huduma ya Stonecroft ikimtegemea Mungu ili kukamilisha mahitaji yote.

Doris Thompson: Makamu wa Raisi

Doris Thompson anawasaidia wanawake kufikia maono yao na mawazo yao katika matendo, akiwa kama makamu wa Raisi, Doris anataka kuwafikia wanawake wengi zaidi katika ulimwengu huu, na anawasaidia wanawake wengi kupitia Stonecroft, na anawasaidia wale wanao jitolea kuwafikia wengine katika maeneo mengi zaidi. Anafanya kazi ya kuibadiri Stonecroft ili iweze kuwafikia watu walio katika maeneo mapya zaidi, Pia kuna watu wengi zaidi katika uongozi ambao hamuwezi kuwa na mawasiliano nao.

Huduma ya Stonecroft inatamani kuwaunganisha wanawake kwa Mungu na kwa wanawake wenzake na katika jamii zao.

Stonecroft inawatia moyo wanawake,kuwa na mawasiliano na wenzao na hata katika jamii zao, na pia kuwaalika katika masomo ya biblia katika vijiji vyao na miji yao.

Haya masomo ni rahisi kuyafuata, na pia ni makundi yanayo leta uzima wa kiroho katika maeneo mkakati wa muda mrefu katika maisha ya waumini.

Hili toleo la kiafrica litaleta matokeo mawili tofauti, la kwanza ni mkakati wa Stonecroft wa kuwafikia wasio fikiwa, na la pili ni mkakati wa Stonecroft wa masomo ya kibiblia. Katika madarasa ya kujisomea biblia, mwongozo wa vitabu vya Stonecroft utatungwa ili kuwa na vikundi vya kujisomea biblia na kuwafikia wasio fikiwa, wasio amini na wanao amini, watatiwa moyo ili wajiunge katika makundi haya .makundi haya yataundwa na wanawake ambao wamemaliza kujisomea vitabu vya “Utatu” lakini hawajafikia kiwango cha kuongoza lakini wanataka kuendelea kujisomea, hili litawezesha ukuwaji na kutanuka kwa stonecroft katika bara la Africa.

Huduma ya Stonecroft inaelewa na kushukuru huduma ya mwanamke mmoja,ukimfikia mwanamke nae akakokoka basi umeweza kuifikia jamii, mume wake, watoto, marafiki, majirani, na anao fanya nao kazi.

Askofu David Akondowi, ambaye ni muwakilishi wa United Caribbean Trust’s (UCT) Tanzania na muasisi wa mafunzo ya wachungaji katika chuo kitwacho Training Bible School (ATBS) na mchungaji wa House of Freedom – Tanzania, ambapo UCT wana mradi wa kuwawezesha wanawake uitwao "Women's Empowerment Sewing Project" yeye anazungumzia juu ya mithari ya Kiswahili isemayo, ’Ukimuwezesha mwanamke umeiwezesha jamii’.

Stonecroft wanawawezesha wanawake ili waweze kufikia jamii zao ki ukamilifu.

 
     
Copyright ©  2023 www.UnitedCaribbean.com. All rights reserved. Disclaimer Click to Contact us