Project Hope     home >> stonecroft>> mwongozo >> somo 4 >> mistari ya biblia
Mistari ya Biblia - Somo #4
Women's Empowerment  Program
Sports Bible Club
Living Water Bible Club

Je Mungu ana nijua?

Mistari ya Biblia

Usomaji wa Biblia wa kila juma

Yohana 6:37
37 Wale wote ambao Baba amenipa watakuja kwangu na ye yote ajaye kwangu, sitamtupa nje kamwe.

Ayubu 34:21
Macho yake yako katika njia za wanadamu, na anaona hatua zake zote.

Zaburi 139:1-6
Ee BWANA umenichunguza na kunijua.
Wewe wajua kuketi kwangu na kuondoka kwangu;
Umelifahamu wazo lanhu tokea mbali.
Umepepeta kwenda kwangu na kulala kwangu, umeelewa na nia zangu zote.
Maana hamna neno ulimini mwangu, usilolijua kabisa BWANA.
Umenizingira nyuma na mbele, ukaniwekea mkono wako.
Maarifa yako ni ya ajabu yanishinda mimi; hayadilikiki ni ya ajabu siwezi kuyafikilia.

Mithari 15:3,11
Macho ya BWANA yako kila mahali,
yakimchunga mbaya na mwema.
Kuzimu na uharibifu vi wazi mbele za BWANA;
Si zaidi basi mioyo ya wanadamu.

2 Nyakati 16:9
Kwa maana macho ya BWANA huzunguka duniani kote, ili ajionyeshe mwenye nguvu kwa ajili ya hao walio kamilika mioyo kuelekea kwake,kwa hayo umetenda upumbavu kwani tangu sasa utakuwa na vita.

Waebrania 13:5
5 Maisha yenu yasitawaliwe na tamaa ya kupenda fedha, na mridhike na mlivyo navyo; kwa kuwa yeye mwenyewe amesema, “Sita kupungukia kamwe wala sitakuacha.”

Yohana 14:21
21 Mtu anayezishika amri zangu na kuziti miza ndiye anayenipenda. Na mtu anayenipenda, Baba yangu atam penda; nami nitampenda na kujidhihirisha kwake.”

Swali #1

Mathayo 18:12-14
12 “Mnaonaje? Kama mtu ana kondoo mia moja na mmoja wao akapotea, hatawaacha wale tisini na tisa mlimani aende kumtafuta yule aliyepotea?13 Na akisha mpata, nawaambia kweli, anafurahi zaidi kwa ajili ya huyo kondoo mmoja kuliko kwa wale tisini na tisa ambao hawakupotea. 14 Hali kadhalika, Baba yenu wa mbin guni hapendi hata mmojawapo wa hawa wadogo apotee.”

Waefeso 2:10
10 Kwa maana sisi ni matokeo ya kazi ya Mungu tulioumbwa katika Kristo Yesu, ili tuwe na matendo mema ambayo Mungu alikwisha andaa, tuishi katika hayo.

Zaburi 100:3
Jueni kwamba BWANA ndiye Mungu;
Ndiye aliye tuumba na sisi tu watu wake;
Tu watu wake na kondoo wa malisho yake.

Swali #4

Zaburi 139:7-18
7 Niende wapi nijiepushe na roho yako? Niende wapi niukimbie uso wako?
8 Kama ningepanda mbinguni, Wewe uko; Ningefanya kuzimu kitanda changu, Wewe uko. 9 Ningezitwaa mbawa za asubuhi, Na kukaa pande za mwisho za bahari; 10 Huko nako mkono wako utaniongoza, Na mkono wako wa kuume utanishika. 11 Kama nikisema, Hakika giza litanifunika, Na nuru inizungukayo ingekuwa usiku; 12 Giza nalo halikufichi kitu, Bali usiku huangaza kama mchana; Giza na mwanga kwako ni sawasawa.
13 Maana Wewe ndiwe uliyeniumba mtima wangu, Uliniunga tumboni mwa mama yangu. 14 Nitakushukuru kwa kuwa nimeumbwa Kwa jinsi ya ajabu ya kutisha. Matendo yako ni ya ajabu, Na nafsi yangu yajua sana, 15 Mifupa yangu haikusitirika kwako, Nilipoumbwa kwa siri, Nilipoungwa kwa ustadi pande za chini za nchi;
16 Macho yako yaliniona kabla sijakamilika; Chuoni mwako ziliandikwa zote pia, Siku zilizoamriwa kabla hazijawa bado.
17 Mungu, fikira zako zina thamani nyingi kwangu; Jinsi ilivyo kubwa jumla yake!
18 Kama ningezihesabu ni nyingi kuliko mchanga; Niamkapo nikali pamoja nawe.

Swali #5

Zaburi 139:23-24
23 Ee Mungu, unichunguze, uujue moyo wangu, Unijaribu, uyajue mawazo yangu; 24 Uone kama iko njia iletayo majuto ndani yangu, Ukaniongoze katika njia ya milele.

Swali #6

Mathayo 6:25-34
25 “Kwa hiyo nawaambia, msiwe na wasiwasi kuhusu maisha yenu: mtakula nini au mtakunywa nini; au kuhusu miili yenu: mvae nini. Kwani maisha si zaidi ya chakula? Na mwili zaidi ya mavazi? 26 Waangalieni ndege wa angani: wao hawapandi wala kuvuna wala kuweka cho chote ghalani. Lakini Baba yenu wa mbinguni anawali sha. Je ninyi, si wa thamani zaidi kuliko ndege?27 Ni nani kati yenu ambaye kwa kujihangaisha kwake anaweza kujiongezea hata saa moja zaidi kwenye maisha yake?

28 “Na kwa nini mnahangaikia mavazi? Angalieni maua ya mwi tuni yanavyostawi. Hayafanyi kazi wala hayashoni nguo. 29 Lakini nawaambia, hata mfalme Sulemani katika ufahari wake wote hakuwahi kuvikwa kama mojawapo la maua hayo. 30 Lakini ikiwa Mungu anay avisha hivi maua ambayo leo yapo na kesho yanatupwa motoni, je, hatawavisha ninyi vizuri zaidi, enyi watu wenye imani haba? 31 Kwa hiyo msiwe na wasiwasi mkisema, ‘Tutakula nini?’ au ‘Tutakunywa nini?’ au ‘Tutavaa nini?’ 32 Mambo haya ndio yanay owahangaisha watu wa mataifa wasiomjua Mungu; na Baba yenu wa mbinguni anafahamu kwamba mnahitaji yote hayo. 33 Lakini uta futeni kwanza Ufalme wa mbinguni na haki yake, na haya yote mtaongezewa. 34 Kwa hiyo msihangaike kuhusu kesho, kwa sababu kesho itajihangaikia yenyewe. Kila siku ina shida zake za kutosha.”

1 Petro 5:6-7
6 Basi, nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu wenye nguvu, ili wakati wake ufaao utakapotimia, awainue.
7 Mwekeeni yeye fadhaa zenu zote kwa maana yeye hujishughul isha sana na mambo yenu.

Mathayo 6:8
8 Msiwe kama wao, kwa sababu Baba yenu anajua mahitaji yenu hata kabla hamjaomba.”

Warumi 8:28-29
28 Tunajua kwamba katika kila kitu Mungu[f] hufanya kazi ili kuwapa mema wale wanaompenda. Hawa ni watu aliowachagua Mungu, kwa sababu huo ndiyo ulikuwa mpango wake. 29 Mungu aliwajua kabla hajauumba ulimwengu. Na aliamua hao wangekuwa kama Mwanaye. Na Yesu angekuwa mzaliwa wa kwanza wa watoto wake wengi.

Swali #7

Zaburi 37:4-5
4 Nawe utajifurahisha kwa Bwana, Naye atakupa haja za moyo wako.
5 Umkabidhi Bwana njia yako, Pia umtumaini, naye atafanya.

MIthari 3:5-6
Umtumaini BWANA kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe; kat ika njia zako zote mkiri yeye, naye atazinyoosha njia zako zote.

Yeremia 29:13
Nanyi mtanitafuta na kuniona mtakapo nitafuta kwa moyo wenu wote.

Swali #9

Yeremia 29:11
Maana najua mawazo niwawaziayo ninyi ni mawazo ya amani asema BWANA, wala si mabaya kuwapa ninyi tumaini katika sku zenu za mwisho.

Swali #10

Warumi 5:6-9
6 Tulipokuwa tungali wanyonge, wakati aliochagua Mungu, Kristo aliwafia wenye dhambi. 7 Ni vigumu sana kwa mtu kujitolea kufa kwa ajili ya mwenye haki, ingawa yawezekana mtu akajitolea kufa kwa ajili ya mtu mwema.8 Lakini Mungu anaudhihirisha upendo wake kwetu kwamba: tulipokuwa tungali wenye dhambi, Kristo ali kufa kwa ajili yetu.
9 Basi, kwa kuwa tumekwisha kuhesabiwa haki kwa damu yake, bila shaka atatuokoa kutoka katika ghadhabu ya Mungu.

Swali #11

Zaburi 147:5
BWANA wetu ni mkuu na mwingi wa nguvu; Akili zake hazina mpaka.

 

 
 

 

The Guide has her own Guidebook to help her lead and guide the lesson.

Download Swahili Lesson #4 Guidebook

Download Swahili Guidebook Bible Verses Lesson #4

JE MUNGU YUKOJE?

Mistari ya Biblia

 
 
Copyright ©  2023 www.UnitedCaribbean.com. All rights reserved. Disclaimer Click to Contact us